MAPISHI YA PILAU LA KUKU

Pilau ni mchanganyiko wa mchele na viungo mbalimbali,chakula hiki ni kitamu sana na watu hupendelea sana kupika wakati wa sherehe. Unaweza ukala pilau na kitoweo chochote kile unachopenda mfano mimi nimependa kula na njegere,kachumbali na matunda.


Mahitaji

  • Mchele
  • Kuku
  • Mafuta
  • Vitunguu maji
  • Carrots
  • Pilipili hoho
  • Tangawizi
  • Viungo vya pilau
  • Vitunguu saumu
  • Chumvi
  • Nyanya 3 

Maelekezo

  • Mkate kuku umpike na chumvi akiiva hakikisha supu ya kupikia chakula inatosha.
  • Menya vitunguu maji ukatekate,vitunguu saumu menya utwange na tangawizi,menya carrots uzikwangue na pilipili hoho ukatekate mwisho nyanya pia menya ukate kate.
  • Bandika sufuria utie mafuta, ikichemka tia vitunguu uvikaange. Vikianza kubadilika rangi weka vitunguu saumu na tangawizi mbichi koroga kidoga weka pilipili hoho na carrots.
  • Kaanga kidogo kisha weka nyanya acha ziive na vipande vya kuku koroga kama dk tano weka viungo vya pilau.
  • Weka mchele koroga kisha tia chumvi na umimine supu ile ya kuku kwenye wali.
  • Koroga kisha funika acha chakula chako kiive baada ya dk kumi angalia chakula chako kama maji yamekauka kigeuze palia baada ya dakika kadhaa angalia tena hapo chakula chako kitakua tayari kuliwa.
  • Pilau yako itakuwa tayari kwa kuliwa
  • Mpendwa wangu karibu mezani

Post a Comment

[blogger]

MKRdezign

Blogger Widgets

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget