Nyama ya ng'ombe ya kukaanga yenye ladha ya kipekee


Mahitaji

  • Nyama  - kilo 1
  • Mafuta ya kula - 1/2 lita
  • Chumvi 
  • Ndimu / limao 1
  • Tangawizi  - 1
  • Kitunguu saumu  - 1
  • Viazi - 6
  • Viungo vingine upendavyo kwenyewaweza kuweka

Maelekezo

  • Tayarisha nyama yako - kata, osha.
  • Weka limao, ndimu au vinegar kwenye nyama, ichanganye ili limao lichanganyike vizuri.
  • Ponda tangawizi kwenye kinu, iwe laini.
  • Ponda kitunguu swaumu kwenye kinu, ilainike vizuri.
  • Weka viungo - chumvi, tangawizi na kitunguu saumu kwenye nyama. Changanya nyama ili viungo vipate kuchanganyika vizuri. Acha nyama ikae kwa dakika 45 kwenye jokofu ili viungo viingie vizuri. Jinsi viungo vinavyokaa vizuri kwenye nyama ndio inazidi kunoga.
  • Bandika sufuria au kikaangio jikoni, weka mafuta kiasi. Subiria yapate moto.
  • Weka nyama kwenye mafuta.  Koroga ili ichanganyike vizuri na mafuta kisha funika sufuria au chungu na mfuniko. 
  • Geuza geuza nyama kila mara ili kuzuia isigande kwenye chombo cha kupikia. Subiria hadi iive.
  • Angalia kama nyama imeiva. Unaweza kuongeza pilipili manga ya unga ili kuleta ladha tofauti kwenye nyama.
  •  Unaweza kutenga na kula.
  •  Ni vizuri ukala kwa kachumbari nzuri pamoja na kinywaji upendacho au chakula chochote ukipendacho

Post a Comment

[blogger]

MKRdezign

Blogger Widgets

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget