WALI WA VIUNGO

Mahitaji


  • Mchele nusu  kg
  • Vitunguu maji 3
  • Karoti 4 kubwa
  • Mafuta
  • Chumvi kiasi upendavyo wewe
  • Pilipili hoho 1
  • Kitunguu saumu 1
  • Pilipili manga nusu kijiko cha chai
  • Iliki iliyosagwa nusu kijiko cha chai

Maelekezo

  • Osha mchele,uache kwenye maji. Menya karoti katakata, vitunguu maji menya ukate kate.
  • Kitunguu saumu menya kiponde na pilipili hoho katakata.
  • Bandika sufuria jikoni, weka mafuta na vitunguu maji koroga kama dakika 2 weka vitunguu saumu, usiache kukoroga.
  • Weka karoto na pilipili hoho, weka iriki na pilipilimanga kisha funika. 
  • Weka mchele na chumvi, weka na maji kama kikombe kimoja na nusu cha chai. 
  • Funika maji yakikauka, usiugeuze ibanike baada ya dakika 10 uangalie, ugeuze onja kama bado una kiini ongeza maji kama vijiko 5 vya chakula. 
  • Funika ukija kuangalia utakua umeiva. 
  • Sasa jilambe.

Post a Comment

[blogger]

MKRdezign

Blogger Widgets

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget