Viazi na meatballs za nazi

Chakula rahisi kuandaa cha viazi na meatballs. Kinapikwa kwa nazi na maziwa. Kinaweza kuliwa na mkate au wali,.

Mahitaji

  • Meatballs 8
  • Nazi ½
  • Maziwa ya mgando 1/8 lita
  • Karoti 1
  • Kitunguu maji 1
  • ½ kijiko cha chai cha chumvi
  • Kijiko 1 cha kitunguu saumu
  • Pilipili hoho ya kijani ½
  • Pilipili hoho nyekundu ½
  • Nyanya 4

Maelekezo

  1. Menya viazi, osha na kisha kata vipande vidogo vidogo. Bandika jikoni na maji ya kutosha. Ongeza chumvi na funika vipate kuchemka, takribani dakika 10 hadi 15.
  2. Injika chungu kwenye jiko tofauti, weka mafuta ya kula mengi na acha yapate moto.
  3. Andaa viungo yako – kitunguu, pilipili hoho, nyanya, karoti na kitunguu saumu.
  4. Mafuta yakipata moto, weka meatballs zako na zigeuze kila baada ya muda hadi ziive vizuri pande zote. Hakikisha zimeiva vizuri ndani. Kisha zitoe na weka kwenye chombo pembeni zipate kupoa.
  5. Viazi vikiiva, ipua na injika sufuria jikoni. Weka mafuta na subiria yapate moto vizuri.
  6. Weka kitunguu maji, koroga kiasi. Ongeza kitunguu saumu huku unaendelea kukoroga hadi vibadilike rangi na kuwa ya udongo iliyopauka.
  7. Ongeza nyanya, koroga. Funika kidogo ipate kuiva na kulainika. Baada ya dakika 5 au 7 ponda nyanya na kisha ongeza viungo vilivyobaki kwa zamu – pilipili hoho, karoti, kisha tui la nazi na mwisho kabisa maziwa kidogo. Koroga na kisha funika vichemke vizuri. Bakisha tui kidogo.
  8.  Sauce yako ikishaiva, ongeza viazi kwenye mchanganyiko, koroga na acha viendelee kuiva. Ongeza tui lililibaki na kisha koroga.
  9. Mchanganyiko ukishaiva, weka meatballs, koroga kiasi, acha ichemke kwa dakika 4 hadi 6 kisha ipua; Usiache muda mrefu sababu nyama italainika sana na kubomoka.
  10. Chakula chako kitakuwa tayari kwa kuliwa

Post a Comment

[blogger]

MKRdezign

Blogger Widgets

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget