Diamond Akabidhiwa Rasmi Leseni ya Wasafi TV na Wasafi Redio



Hatimaye Bosi wa Wasafi Classic Baby (WCB) Diamond Platinumz amepata leseni ya kuziweka hewani redio na televisheni za Wasafi zilizobatizwa jina la ‘Wasafi Radio na Wasafi TV’.

Diamond amevuka maji na kuzipata leseni zake visiwani Zanzibar ambapo alikabidhiwa na Wizara ya Habari, Tamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar, Rashid Ali Juma.

Mkali huyo wa ‘Sikomi’ jana aliwashirikisha mashabiki wake habari hiyo njema iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu, siku chache baada ya kuonesha picha akiwa anajaribu mitambo ya mradi huo mpya.

Kupitia Instagram, ameandika ujumbe akiambatanisha na picha za leseni hizo, akiishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Post a Comment

[blogger]

MKRdezign

Blogger Widgets

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget