May 2018



Mwanadada Irene Uwoya na mume wake Dogo Janja ambao kila siku hawaishiwi na drama katika  mitandao wanakuja tena kivingine na kuelezea jinsi mwezi mtukufu wa Ramadhani unavyodumisha mahusiano katika ndoa yao.

Irene anasema kuwa akiwa kama mke halali wa Abdul (janjaro) anahaki zote za kukaa na kutulia kipindi hiki cha ramadhan na kumpikia mume wake  kwa sababu hicho ni kitu alichozoea hata katika ndoa yake iliyopita.
 
"Kuhusu kufunga kwa upande wangu nilishazoea kwa sababu hata siku za nyuma za ramadhani nilikuwa nikifanya hivyo hivyo nilipokuwa na Ndiku na kwa sababu sasa hiv mimi ni mke halali kabisa wa Abdul basi nina haki ya kutulia na kumpikia mume wangu futari."-Uwoya




Mwanamuziki wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money ameomba radhi baada ya ugomvi wake na Baba mtoto wake Mo J.

Gigy Money alimtolea maneno makali Ex wake ikiwemo kuweka wazi kwenye Interview aliyofanya na Millard Ayo kuwa mtoto wake Myra sio wa Mo J kwani alikuwa na mwanaume mwingine.

Gigy Money na Ex wake Mo J walirushiana maneno makali baada ya Gigy kumtuhumu kuwa hakuwa akimtunza kipindi cha ujauzito na kudai alihama na kila kitu baada ya kuachana.

Baada ya sakata hilo Mo J aliongea na vyombo vya habari na kudai kuwa ana uhakika kuwa mtoto wao ni wa kwake ingawa Gigy kwa ajili ya hasira anampa  mtoto mpenzi wake wa sasa.

Baada ya povu hilo Gigy Money ameibuka na kuomba radhi kwa maneno aliyoongea huku akidai ilikuwa ni hasira

MKRdezign

Blogger Widgets

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget